Mmiliki wa Facebook afanya ziara ya kushitukiza kwa familia moja jimbo la ohio.

                          Mack Zuckerberg akipata mlo wa pamoja na familia aliyoitembelea.

Mwanzilishi na mmiliki wa mtandao ya kijamii unaotajwa kuwa na watumiaji wengi duniani yaani facebook Mack Zuckeberg ameripotiwa kuitembelea familia moja inayoishi Newton Falls nchini Marekani ambapo alifanya hivyo kwa kushitukiza pasipo kuwapa taarifa rasmi ya ujio wake.

Kwa mujibu wa ripoti za vyombo vya habari vya nchini marekani ni kuwa familia hiyo ilipata taarifa ya ujio wa Zuckerberg katika nyumba yao Dakika ishirini kabla.

Bwana Zuckerberg amefanya hivyo ikiwa ni katika mpango wake wa kutembelea majimbo yapatayo hamsini ya nchini marekani.

Comments