N'Golo Kante aibuka mshindi tuzo ya PFA Uingereza

                                                                 N'golo Kante
Kiungo wa klabu ya Chelsea Ngolo Kante ametwaa tuzo ya mchezaji bora wa mwaka wa chama cha wachezaji wa kulipwa nchini England PFA kwa msimu wa 2016-17.
Kante amewapiku nyota wengine wa ligi hiyo Eden Hazard, Harry Kane, Romelu Lukaku, Zlatan Ibrahimovic na Alexis Sanchez waliokua wakiwani tuzo hiyo pia.
                                                             Dele Alli
Kiungo wa Tottenham Dele Alli, ameshinda tuzo ya mchezaji bora chipukizi kwa mwaka wa pili mfululizo. na kuwapiku Michael Keane wa Burnley, Romelu Lukaku, kipa wa Sunderland Jordan Pickford na Leroy Sane wa Manchester City walikua wakiwani tuzo hiyo ya mchezaji chipukizi wa mwaka.
Lucy Bronze wa Manchester City ameshinda tuzo ya mchezaji bora wa kike wa mwaka katika hizo, huku Jess Carter anayechezea Birmingham ameibuka kidedea kwa kuwa chipukizi bora kwa upande wa wanawake.
                                             (Taarifa kutoka Tovuti ya bbc swahili)

Comments