R.KELLY MEDIA YAMPACHIKA ALI KIBA JINA LA "KING OF TANZANIA"

Mwaka 2014 huenda ukawa na maana kubwa zaidi kwa Ali Kiba kwani licha ya kufanya poa na material yake kali ya "Mwana" na kufunika mbaya katika matamasha makubwa aliyopata nafasi ya kuperform bado nyota yake imeonekana kupata nuru zaidi hiyo ni mara baada ya kambi inayomsampoti mkali R.kelly wa marekani inayojiita
R.kelly Media kuibuka kupitia mitandao mbalimbali ya kijamii na kuonyesha kumpa sapoti ya nguvu "mwana" Ali Kiba kwa kumpachika jina la "KING OF TANZANIA" hata hivyo bado haijafahamika wazi kama kambi hiyo ipo chini ya R.kelly au ni mashabiki tu wenye love ya kutosha kwa R.Kelly.
Kwa wenye kumbukumbu nzuri ya matukio ya kiburudani watakumbuka tukio la mwaka 2010 la Airtel One8 ambalo lilikuwa likisimamiwa na R.Kelly ambapo aliandika wimbo na kushirikisha wasanii wakali kutoka Afrika akiwemo 2Face Idibia wa Nigeria,Amani(Kenya),Navio (Uganda) Fally Ipupa pamoja na Aly Kiba kutoka TZ.

Comments