CHRISS BROWN ATOA KIPANDE CHA VIDEO AKIONGELEA MAHUSIANO YAKE NA WANADADA RIHANA NA KARUECHE

 Baada ya siku chache zilizopita mtu mzima Chriss Brown kutangaza kuachana na aliyekuwa mpenzi wake Karrueche Tran ili kuimarisha mapenzi yake na mwanadada Rihana Robin Fenty a.k.a Rih-Rih,saga linaendelea kwa Chriss Brown kuibuka  na kutoa kipande kifupi cha video akiongelea mahusiano ya kimapenzi na warembo hao wawili katika kipindi kimoja,
kipande hicho cha video kimedairektiwa na David Allan,ambapo Chriss alijiachia kwa kusema nina stress nyingi sababu unakuwa kwenye mahusiano na mtu mnashare historia na vitu vingi lakini ghafla unajikuta unaangukia kwa mtu mwingine,ni ngumu sana kuwa na wapenzi wawili kwa wakati mmoja sipendi kumuumiza yeyote, mimi siyo player mama yangu hakunifunza niwe hivyo alifunguka mtu mzima Chriss Breezy.


Comments